AZMA ni mmoja wa wasanii wakubwa wa HIP HOP nchini Tanzania mwenye maskani yake jijini Dar es Salaam, mara tu baada ya jamaa huyu kuachia video yake ya wimbo wake mpya ( KUWA NA AZMA)
nilifanya jitihada ya kumtafuta ili kujua nini jamaa amezungumzia kwenye wimbo huo, kupitia Whatsup niliweza kuchart nae poa na hivi ndivyo jamaa alisema kuhusu wimbo wake huo na jinsi alivyouhusianisha na jina lake
AZMA alisema " AZMA maana yake ni lengo/ dhumuni au nia ya kufanya kitu fulani, na hili jina ni jina langu kabisa la darasani nililopewa na wazazi kwani wao waliniita AZIMA lakini kutokana na ukali wa jina hili nivyofika darasa la tatu (3) nilibadili jina na nikajiita AZMA "
Na nilipo muuliza nini uhusiano kati ya jina lake na jina la wimbo wake mpya ( KUWA NA AZMA) AZMA alisema ," KUWA NA AZMA au kuwa na nia,nimeandika huu wimbo kama dedication kwa watu wote,wanao pambana kutafuta maisha, Maisha yana vikwazo sana,tunatapaswa kuwa na AZMA(NIA) ya dhati, katika kufanya jambo lolote, vikwazo ni sehemu ya maisha, tusikate tamaa, kwa kuwa VIKWAZO(challenges) vipo ili kuonyesha ni kiasi gani tupo STRONG"
Ahsante kwa kutembelea blog yetu kuwa mwanafamilia kwa kutu follow
Facebook - like page yetu @ Agu Classic
Twitter - @ AugustinoDamson
Facebook - @ Augustino Kaulule
Instagram - @ aguclassic
Whatsup - 0753825788
No comments:
Post a Comment